Isaiah 24:1-3

Dunia Kuharibiwa Upesi

1 aTazama, Bwana ataifanya dunia kuwa ukiwa
na kuiharibu,
naye atauharibu uso wake
na kutawanya wakaao ndani yake:
2 bndivyo itakavyokuwa
kwa makuhani na kwa watu,
kwa bwana na kwa mtumishi,
kwa bibi na kwa mtumishi wake wa kike,
kwa muuzaji na kwa mnunuzi,
kwa mkopaji na kwa mkopeshaji,
kwa mdaiwa na kwa mdai.
3 cDunia itaharibiwa kabisa
na kutekwa nyara kabisa.
Bwana amesema neno hili.
Copyright information for SwhNEN